Health Encyclopedia
A B C D E F G H I J K L M N O P Q R S T U V W X Y Z A-Z Listings

Uchunguzi wa Hali ya Mtoto: Hadi Mwezi 1

Baada ya ziara yako ya kwanza ya mtoto aliyezaliwa, huenda mtoto wako akafanyiwa uchunguzi ndani ya mwezi wake wa kwanza maishani. Kwenye uchunguzi huu, mtoa huduma wa afya atamchunguza mtoto na kuuliza jinsi mambo yanavyoendelea nyumbani. Fomu hii inaelezea baadhi ya kile unachoweza kutarajia.

Ukuaji na uwezo

Mtoa huduma wa afya atauliza maswali kuhusu mtoto wako. Atamwangalia mtoto wako ili kupata habari kuhusu ukuaji wake. Kwa ziara hii, kuna uwezekano mtoto wako anafanya baadhi ya yafuatayo:

  • Anatabasamu bila sababu yoyote (inaitwa “tabasamu ya hiari”)

  • Kukazia macho haswa anaponyonya

  • Kutoa sauti bila mpangilio (pia huitwa “kupiga kelele”)

  • Kujaribu kuinua kichwa chake

  • Kugaagaa na kunyonganyonga mwili. Kila mkono na mguu unapaswa kusonga takribani hatua sawa. Ikiwa sivyo, mwambie mtoa huduma wa afya.

  • Kushtuka anaposikia kelele

 

Vidokezo vya kulisha

Takribani umri wa wiki 2, mtoto wako anapaswa kurejesha uzito wake aliokuwa nao alipozaliwa. Endelea kumpa mtoto wako maziwa ya mama au fomula. Ili kumsaidia mtoto wako ale vizuri:

  • Mlishe mtoto wako mara kwa mara na wakati anapotaka. Hakikisha kuwa unanyonyesha angalau mara 8 hadi 12 kwa siku. Huenda baadhi ya milo hii ikakaribiana (mlo wa mkusanyiko) na kisha huenda mtoto wako akapumzika kwa saa kadhaa. Mruhusu mtoto wako anyonye atakavyo. Anapokamilisha ataacha kumeza, atatuliza mikono yake na kulala.

  • Usiku, mlishe mtoto anapoamka, mara nyingi kila baada ya saa 3 hadi 4. Unaweza kuamua kumwamsha mtoto kwa milo ya usiku. Jadili hili na mtoa huduma wa afya.

  • Mnyonyeshe kwa takribani dakika 15-20 kila wakati. Ukitumia chupa, ongeza polepole kiasi cha fomula au maziwa ya mama unayompa mtoto wako. Watoto wengi hula aunsi 4 (mililita 118) kwa kila mlo kufikia umri wa mwezi 1, lakini hali hii inaweza kutofautiana.

  • Ikiwa una wasiwasi kuhusu kiasi au mara ambazo mtoto wako anakula, mwambie mtoa huduma wa afya.

  • Mwulize mtoa huduma wa afya ikiwa mtoto wako anapaswa kupata vitamini D.

  • Usimpe mtoto mlo wowote isipokuwa maziwa ya mama au fomula. Mtoto wako ni mchanga sana kuweza kula vyakula vigumu au vioevu vingine. Mtoto mchanga wa umri huu hahitaji kupewa maji.

  • Fahamu kuwa watoto wengi huanza kutema wakiwa na takribani umri wa mwezi 1. Mara nyingi hii ni hali ya kawaida. Wasiliana na mtoa huduma mara moja mtoto akitema mara kwa mara kwa nguvu, au akitema chochote ambacho si maziwa wala fomula.

 

Vidokezo vya usafi

  • Watoto wengine huenda haja kubwa (choo) mara chache kwa siku. Wengine huenda haja mara moja kila baada ya siku 2 hadi 3 . Chochote kinachohusiana na hili ni kawaida. Badilisha nepi kila inapokuwa na unyevu au chafu.

  • Ni sawa ikiwa mtoto wako anaenda haja kubwa mara chache kuliko kila baada ya siku 2 hadi 3 ikiwa mtoto ana afya nzuri. Lakini ikiwa mtoto anasumbuka, anatema zaidi ya kawaida, anakula kidogo kuliko kawaida, au ana choo kigumu sana, mwambie mtoa huduma wa afya. Huenda mtoto hapati choo. Hii inamaanisha mtoto ameshindwa kuenda haja kubwa.

  • Choo kinaweza kuwa cha rangi ya manjano hadi hudhurungi hadi kijani. Ikiwa choo ni cha rangi nyingine, mwambie mtoa huduma wa afya.

  • Mwogeshe mtoto wako mara chache kwa wiki. Mwogeshe mara kwa mara ikiwa mtoto anafurahia. Lakini kwa sababu unasafisha mtoto wakati wa kubadilisha nepi, huhitaji kumwogesha kila siku.

  • Ni Sawa kutumia krimu kidogo au losheni kwenye ngozi ya mtoto. Usiweke losheni kwenye mikono ya mtoto.

 

Vidokezo vya kulala

Katika umri huu, mtoto wako anaweza kulala takribani saa 18 hadi 20 kila siku. Ni kawaida kwa watoto kulala kwa muda mfupi siku nzima, badala ya saa kwa wakati. Huenda mtoto akawa anahangaika kabla ya kuenda kulala usiku (takribani saa 6 jioni hadi saa 9 usiku). Hii ni hali ya kawaida. Ili kumsaidia mtoto wako kulala salama na vizuri:

  • Mweke mtoto mchanga alale kwa mgongo wake kwa usingizi kidogo na kulala hadi afikishe mwaka 1. Hii inaweza kupunguza hatari ya SIDS (dalili za kifo cha ghafla cha mtoto mchanga) mpumuo na kusakamwa. Usiwahi kumlaza mtoto upande wake wala kwa tumbo kwa usingizi mrefu au mfupi. Ikiwa mtoto ameamka, mpe muda alale kwa tumbo mradi tu uwe unamwangalia. Hii husaidia mtoto kuwa na misuli thabiti ya tumbo na shingo. Pia hii itasaidia kupunguza kichwa cha mtoto wako kuwa bapa. Tatizo hili linaweza kutokea wakati watoto wanatumia muda mwingi kulala kwa migongo yao.

  • Mwulize mtoa huduma wa afya ikiwa unapaswa kumruhusu mtoto wako kulala na titibandia. Kulala na titibandia kumeonyesha kupunguza hatari ya SIDS. Lakini usimpe hadi baada ya kukamilisha kunyonya. Ikiwa mtoto wako hataki titibandia, usijaribu kumlazimisha atumie.

  • Usiweke hori, mto, mablanketi yaliyolegea, au wanyama bandia katika hori. Vitu hivi vinaweza kumkosesha mtoto hewa.

  • Usimweke mtoto wako kwenye kochi wala kiti cha mikono ili kulala. Kulala kwenye kochi au kiti cha mikono humweka mtoto kwenye hatari zaidi ya kifo, ikiwemo SIDS.

  • Usitumie viti vya mtoto mchanga, viti vya gari, vitembezi, keria za watoto wachanga au bembea za mtoto mchanga kwa kulala mara kwa mara na usingizi kidogo wa kila siku. Hatua hizi zinaweza kusababisha uzuiaji wa njia ya hewa au mtoto kukosa hewa.

  • Kumfungia mtoto kwenye blanketi (kumfunga mtoto) kunaweza kusaidia mtoto wako kuhisi salama na kulala. Hakikisha kuwa mtoto wako anaweza kusogeza miguu yake kwa urahisi. Acha kumfungia pindi tu mtoto wako anapoanza kujifunza jinsi ya kubingiria.

  • Ni Sawa kumlaza mtoto akiwa hajalala. Pia ni Sawa kumwacha mtoto alie akiwa kitandani, lakini kwa dakika chache tu. Katika umri huu, watoto hawako tayari “kulia wenyewe hadi walale.”

  • Ikiwa unatatizika mtoto wako kulala, mwulize mtoa huduma wa afya vidokezo.

  • Usishiriki kitanda (kulala pamoja) na mtoto wako. Kulala kwenye kitanda kimoja kumeonyesha kuongeza hatari ya SIDS. American Academy of Pediatrics (AAP) inapendekeza kuwa watoto wachanga walale kwenye chumba kimoja na wazazi wao. Wanapaswa kuwa karibu na kitanda cha wazazi wao, lakini katika kitanda tofauti au hori bora. Mpangilio huu wa kulala unapaswa kufanywa kwa mwaka wa kwanza wa mtoto, ikiwezekana. Lakini unapaswa kufanya hivyo kwa angalau miezi 6 ya kwanza.

  • Weka hori, matenga ya watoto na yadi za kucheza katika maeneo yasiyo na hatari. Hii inamaanisha kusiwe na kamba, nyaya, au mapazia ya dirisha yanayoning`inia. Hii itapunguza hali ya kujinyonga.

  • Usitumie mapigo ya moyo ya mtoto na monita au vifaa maalum kusaidia kupunguza hatari ya SIDS. Vifaa hivi vinajumuisha kabari, vishikaji nafasi na magodoro maalum. Vifaa hivi havijathibitisha kuzuia SIDS. Vimesababisha kifo cha mtoto mchanga kwa nadra sana.

  • Zungumza na mtoa huduma wa afya wa mtoto wako kuhusu masuala haya na mengine ya afya na usalama.

 

Vidokezo vya usalama

Mwanamke akimweka mtoto kwenye keria.
Ni sawa kumpeleka mtoto nje. Epuka kumweka kwenye jua kwa muda mrefu na umati ambapo viini vinaweza kusambaa.
  • Ili kuzuia michomo, usibebe wala kunywea vioevu moto kama vile kahawa karibu na mtoto. Punguza halijoto ya kichemshio cha maji hadi 120°F (49°C) au chini.

  • Usivute wala kuruhusu wengine wavute sigara karibu na mtoto. Ikiwa wewe au wanafamilia wengine wanavuta sigara, vutia nje ukiwa umevaa jaketi na kisha uvue jaketi kabla ya kumshika mtoto. Usiwahi kuvuta sigara karibu na mtoto.

  • Kwa kawaida ni sawa kumpeleka mtoto nje. Lakini kaa mbali na maeneo yeliyobanana na kujaa watu ambapo viini vinaweza kusambaa.

  • Unapompeleka mtoto nje, usikae muda mrefu sana kwenye mwangaza wa jua wa moja kwa moja. Mfunike mtoto au nenda kwenye kivuili.

  • Mweke mtoto kwenye kiti cha gari kinachoangalia nyuma ukiwa garini kila mara. Hii inapaswa kuwekwa kwenye kiti cha nyuma kulingana na maelekezo ya kiti cha gari. Usiwahi kumwacha mtoto peke yake garini.

  • Usimwache mtoto wako kwenye sehemu ya juu, kama vile meza, kitanda wala kochi. Anaweza kuanguka na kuumia.

  • Huenda ndugu wakubwa wakataka kumshika, kucheza naye na kutaka kumjua mtoto. Hii ni sawa mradi tu mtu mzima anaangalia.

  • Wasiliana na mtoa huduma wa afya mara moja ikiwa mtoto wako ana homa (tazama Homa na watoto, hapa chini).

 

Chanjo

Kulingana na mapendekezo kutoka CDC, mtoto wako anaweza kupata chanjo ya homa ya ini B ikiwa bado hakupata hospitalini baada ya kuzaliwa. Kumpa mtoto wako chanjo zote pia kutasaidia kupunguza hatari SIDS kwa mtoto wako.

 

Homa na watoto

Tumia kipimajoto cha dijitali kuangalia halijoto ya mtoto wako. Usitumie kipimajoto za zebaki. Kuna aina tofauti na matumizi ya vipimajoto vya dijitali. Vinajumuisha:

  • Rektamu. Kwa watoto walio chini ya miaka 3, halijoto ya rektamu ni sahihi zaidi.

  • Paji la uso (panja). Hii hufanya kazi kwa watoto walio na umri wa miezi 3 na zaidi. Ikiwa mtoto chini ya miezi 3 ana dalili za ugonjwa, hii inaweza kutumiwa kwa pasi ya kwanza. Mtoa huduma anaweza kutaka kuthibitisha kwa halijoto ya rektamu.

  • Sikio (kiwambo cha sikio). Halijoto za sikio ni sahihi baada ya umri wa miezi 6, lakini si kabla.

  • Kwapa (kwapajani). Hii ndiyo inayoaminika kidogo lakini inaweza kutumiwa kwa pasi ya kwanza kuangalia mtoto wa umri wowote aliye na ishara za ugonjwa. Mtoa huduma anaweza kutaka kuthibitisha kwa halijoto ya rektamu.

  • Mdomo. Usitumie kipimajoto ndani ya kinywa cha mtoto wako hadi awe na miaka 4.

Tumia kipimajoto cha rektamu kwa uangalifu. Fuata maelekezo ya mtengenezaji bidhaa kwa matumizi sahihi. Kiweke taratibu. Kiweke lebo na uhakikishe hakijatumiwa mdomoni. Huenda kikapita kwenye viini kutoka kwenye choo. Ikiwa unahisi si Sawa kutumia kipimajoto cha rektamu, mwulize mtoa huduma wa afya aina ya kutumia badala yake. Ukizungumza na mtoa huduma yeyote wa afya kuhusu homa ya mtoto wako, mwambie aina uliyotumia.

Hapa chini pana miongozo ya kujua ikiwa mtoto wako ana homa. Mtoa huduma wa afya wa mtoto wako anaweza kukupa nambari tofauti za mtoto wako. Fuata maagizo mahususi ya mtoa huduma wako.

Vipimo vya homa vya mtoto chini ya miezi 3:

  • Kwanza, mwulize mtoa huduma wa afya wa mtoto wako jinsi unavyopaswa kupima halijoto.

  • Rektamu au paji la uso: 100.4°F (38°C) au juu zaidi

  • Kwapa: 99°F (37.2°C) au juu zaidi

Vipimo vya homa vya mtoto wa miezi 3 hadi miezi 36 (miaka 3):

  • Rektamu, paji la uso, au sikio: 102°F (38.9°C) au juu zaidi

  • Kwapa: 101°F (38.3°C) au juu zaidi

Wasiliana na mtoa huduma wa afya katika hali hizi:

  • Halijoto ya kurudia ya 104°F (40°C) au juu zaidi kwa mtoto wa umri wowote

  • Homa ya 100.4° (38°C) au juu zaidi kwa mtoto chini ya miezi 3

  • Homa inayodumu zaidi ya saa 24 kwa mtoto chini ya miaka 2

  • Homa inayodumu kwa siku 3 kwa mtoto wa miaka 2 au zaidi

 

Ishara za mfadhaiko wa baada ya kujifungua

Ni kawaida kutaka kutoa machozi na kuchoka baada ya kujifungua. Hisia hizi zinapaswa kutoweka baada ya wiki moja. Ikiwa bado unahisi hivi, huenda ikawa ishara ya mfadhaiko wa baada ya kujifungua, tatizo baya zaidi. Dalili zinaweza kujumuisha:

  • Hisia za huzuni nyingi

  • Kuongeza au kupoteza uzito

  • Kulala sana au kidogo sana

  • Kuhisi kuchoka kila wakati

  • Kuhisi kutotulia

  • Kuhisi kukosa maana au kuwa na hatia

  • Kuogopa kuwa mtoto atadhuriwa

  • Kuhofia kuwa wewe ni mzazi mbaya

  • Kutatizika kufikiria vizuri au kufanya maamuzi

  • Kufikiria kuhusu kifo au kujitia kitanzi

Ikiwa una dalili yoyote kati ya hizi, zungumza na OB/GYN wako au mtoa huduma mwingine wa afya. Tiba inaweza kukusaidia kuhisi vizuri.

Uchunguzi unaofuata kwenye: _______________________________

MADOKEZO YA MZAZI:

Powered by
Disclaimer